Friday, April 27, 2012

Tundu Lisu

Tundu Lisu ashinda kesi

Hukumu ya LIssu leo

Hukumu Ya Lissu- Updates

Hoja tatu za kwanza zimetupwa,sasa jaji anafafanua ya nne kuwa Lissu alihonga vyakula mawakala isipokuwa wa CCM pekee.hoja ziko tisa tuendelee kufatilia
Updates
Hata hoja ya nne imetupwa

Sherehe za MUUNGANO WA TANZANIA BARA NA VISIWANI


Magazeti Leo Ijumaa




'





Kijitonyama Lutheran centre

Kijitonyama Lutheran Centre Kuzinduliwa

Jengo la kitega uchumi cha KKKT Kijitonyama litazinduliwa tar 29.4.2012. Ujenzi wa jengo hilo umegharimu shilingi bilioni 3.5
Picha kwa hisani ya MICHUZI

SHEREHE ZA MUUNGANO APRILI 26

SHEREHE ZA MUUNGANO LEO


 Rais Dk. Jakaya Kikwete, akipunga mkono kusalimia wananchi wakati akiingia Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo Aprili 26, 2012 katika sherehe za miaka 48 ya Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
 Rais Kikwete akikagua gwaride

 Rais Kikwete akimsalimia Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba
 Rais Kikwete akimsalimnia Mama Maria Nyerere. Kulia ni Spika wa Bunge Anna Makinda
 Baadhi ya Viongozi wa Kiserikali wakiwa ni miongoni mwa waliohudhuria sherehe hizo katika Uwanja wa Uhuru, wakisimama wakati wa kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
 Rais Kikwete akimsalimia Makamu wake, Dk. Mohammed Gharib Bilal
 JWTZ wakionyesha ukakamavu wao wakati wa gwaride
 Nevi katika gwaride
 Vijana wa halaiki wakisherehesha maadhimisho hayo
Kikundi cha Sanaa cha JKT Oljoro, kikionyesha umahiri wake wa kuimba na kucheza 'Kiduku' wakati wa sherehe hizo. Picha: Freddy Maro na Muhidin Sufian

SHULE NA VIBOKO

Kiboko Kinaweza Kuondolewa Kwenye Malezi Ya Mtoto?

Reactions::

Wasikilize Wabunge Walioanguka Saini Za Kumng'oa Pinda!

video


Charles Taylor Alifadhili Vita Sierra Leone

Charles taylor akiwa mahakamani
Majaji katika mahakama maalum ya kimataifa wamempata na hatia Rais wa zamani nchini Liberia Charles Taylor na hatia ya kufadhili vita nchini Sierra Leone.
Taylor ameshtakiwa mbele ya mahakama maalum inayochunguza uhalifu wa kibinadamu nchini Sierra Leone.
Kesi dhidi ya kiongozi huyu imechukua takriban miaka mitano.
Taylor alituhumiwa kwa kuwaunga mkono waasi ambao waliwaua maelfu ya raia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sierra Leone kati ya mwaka 1991-2002.
Hata hivyo mahakama haijampata na hatia ya kuamrisha kutekelezwa kwa uhalifu wowote.
Jaji mwandamizi wa kesi ya Charles Taylor Richard Lussick amesema mahakama inao ushahidi kwamba Taylor alifadhili kwa hali na mali maasi ya nchi jirani ya Sierra Leone.
chanzo:BBC

Thursday, April 26, 2012

TGNP Yaitaka Serikali Iwajibishe Mawaziri Wabadhirifu


TGNP Yaitaka Serikali Iwajibishe Mawaziri Wabadhirifu

Na Mwandishi Wetu

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP) imeitaka Serikali kuwawajibisha mara moja mawaziri, manaibu waziri na watendaji wakuu wa Serikali na mashirika ya umma ambao wametajwa kuhusika na matumizi mabaya ya fedha za umma ama kushindwa kusimamia rasilimali za taifa.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Anna Kikwa katika taarifa yake aliyoisambaza kwa vyombo vya habari. Aidha amemtaka mkuu wa nchi awafute kazi watendaji wanaotumia vibaya fedha za umma na kuwaongezea wananchi umasikini, ili iwe fundisho kwa watendaji wa Serikali wenye tabia kama hiyo na wachukuliwe hatua za kisheria.

Hata hivyo TGNP imeishauri Serikali kuboresha mifumo ya kusimamia rasilimali za nchi yetu ili wananchi wote waweze kufaidi keki ya taifa kwa sababu mara zote Serikali imekuwa ikisema Tanzania hatuna rasilimali lakini hali halisi ni kwamba rasilimali za taifa zinaliwa na mafisadi wachache wa ndani na nje ya nchi.
Katika hatua nyingine, mtandao huo umetoa pongezi kwa wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu, Ardhi Maliasili na Utalii kwa kusimamia vema na kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazotokana na walipa kodi na kuwasilisha ripoti zao Bungeni ambazo zimeibua uozo mkubwa na kujenga mjadala mpana unaotaka uwajibikaji kwa wanaohusika.
“Tunawapongeza pia baadhi ya wabunge  walioshiriki katika mijadala  kwa kuzijadili ripoti hizo kwa undani bila kujali urafiki, itikadi za kisiasa, hasa ile ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa  kuibua  uozo uliojificha na kusimamia maslahi ya Taifa.” amesema Bi. Kikwa katika taarifa hiyo.
“Tumeshuhudia mara kadhaa kupitia vyombo vya habari  wabunge wakiacha itikadi zao za kisiasa na kusimamia kwa dhati dhana ya kushinikiza uwajibikaji katika vyombo vinavyohusika kutokana na ufisadi kama Richmond, Dowans nk. Hata hivyo, TGNP kwa muda mrefu tumekuwa tukipinga ubadhirifu wa fedha za umma  na kudai haki ili kutokomeza ufisadi uliokithiri, lakini bado ufisadi umezidi kushamiri hasa katika Wizara na taasisi za umma.
“Sisi kama wanaharakati tunasema kuendelea kwa ufisadi ni aibu kwa serikali iliyoko madarakani, TGNP tuko mstari wa mbele  kushinikiza rasilimali za taifa ziwanufaishe wananchi wote, hasa walioko pembezoni, kamwe hatutanyamazia aina yoyote ya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya wananchi zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.” Imesema taarifa hiyo.
"Tumeshuhudia wanawake na wasichana wakiendelea kuwa maskini na kukumbana na mifumo kandamizi kwa kukosa haki za kufikia huduma za msingi kama vile maji, barabara, afya, elimu, kilimo, utawala bora n.k. Fedha zinazopotea zinatokana na kodi za wananchi na jamii ina haki ya kuhoji uwajibikaji na wahusika wanatakiwa kuchukuliwa  hatua za kisheria," imeongeza taarifa hiyo kwa vyombo vya habari.
Vilevile tunawapongeza wabunge wote walioshiriki kwa dhati katika zoezi la kusaini kusudio la kutaka viongozi waliotajwa/kutuhumiwa  kwenye ripoti hizo kuwajibika. Ili kuonesha dhana ya uwajibikaji na utawala bora unaozingatia misingi ya haki za binadamu.
Kutoka Fullshangwe

Waziri Akiri Kununua Nyumba Ya Mamilioni


Waziri Akiri Kununua Nyumba Ya Mamilioni


NI EZEKIEL MAIGE, ADAI ALIINUNUA KWA DOLA 410,00, LEMBELI APINGA, ASEMA ALIINUNUA KWA DOLA 700,000 TASLIMU
Fidelis Butahe na Daniel Mjema
SIKU chache baada ya gazeti hili kuripoti taarifa za uchunguzi kwamba kuna mawaziri wawili ambao wamenunua nyumba mbili zenye thamani ya Sh1.8 bilioni, mmoja wa mawaziri hao, Ezekiel Maige wa Maliasili na Utalii ameibuka na kukiri.Maige aliliambia gazeti hili jana kuwa nyumba yake hiyo iliyoko Mbezi Beach, Dar es Salaam, ameinunua kwa Dola za Marekani 410,000 (takriban Sh656 milioni) ambazo anadai kuwa ni mkopo kutoka Benki ya CRDB.

Waziri wa Maliasili na Utalii,Ezekiel Maige
Hata hivyo, wakati Waziri Maige akieleza kuwa nyumba hiyo ina thamani hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli amedai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba ilinunuliwa kwa fedha taslimu Dola 700,000 za Marekani (takriban Sh1.1 bilioni).

Awali, habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa Waziri Maige alinunua nyumba hiyo kutoka kwa Kampuni ya Savana Real Estate.

Mmoja wa madalali wanaouza nyumba za kampuni hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Athuman (Ustadhi) alilithibitishia gazeti hili kwamba Waziri Maige amenunua nyumba moja kati ya nne zilizoko sokoni.

Hata hivyo, dalali huyo hakutaka kueleza alinunua nyumba hiyo lini na kwa gharama gani baada ya kueleza kuwa yeye si msemaji wa kampuni hiyo.

“Nyumba zipo nne na mbili zimeshauzwa. Maige kanunua nyumba moja. Nyumba nyingine mbili bado hazijauzwa na kwa sasa tunamalizia kuziwekea milango na bustani,” alisema Athuman.

Akizungumza na gazeti hili jana, Waziri Maige alisema hakununua nyumba hiyo kwa Dola 700,000 kama inavyodaiwa, bali alinunua kwa Dola za Marekani 410,000.Mbali ya kukiri, alifafanua jinsi alivyoinunua na kuonyesha nyaraka mbalimbali huku akieleza kuwa sehemu ya fedha alizonunulia, zilikuwa za mkopo kutoka Benki ya CRDB.

Alisema mwaka 2005 alipoanza kuwa mbunge alipata mkopo na yeye na wenzake watatu, waliunda kampuni ya kusafirisha mzigo ya Splendid Logistic na kuanza kununua magari matatu na baadaye magari hayo yaliongezeka na kufikia saba.

Soma zaidi:http://www.mwananchi.co.tz

Wednesday, April 25, 2012

KESHO SIKU YA MUUNGANO WA TANZANIA NA ZANZIBAR

Na Heri Shaaban
 
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kuwa mgeni rasmi katika madhimisho ya miaka 48 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zitakazofanyika katika uwanja wa Uhuru Dar es Salam.
 
 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam jana,Bi.Mwamtumu Mahiza alisema kuwa sherehe hizo zitaanza majira ya saa mbili asubuhi ambapo milango ya uwanja huo itafunguliwa kuanzia saa 12 asubuhi.
 
 ''Sherehe hizi za kiistoria za Muungano zilizo asisiwa na waasisi wetu Baba wa Taifa Julius Nyerere na Hayati Habeid Amani Karume zinatarajia kufana"alisema Bi Mahiza.
 
 
Alisema kuwa  viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wataudhuria sherehe hizo akiwemo Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.Mohamed Shein. 
 
Alisema kuwa katika kipindi cha miaka 48 Serikali imepata mafanikio makubwa ya kujivunia  katika nyanja mbalimbali zikiwemo za maendeleo ya jamii,uchumi,siasa ulinzi,usalama pamoja na uhusiano wa kimataifa.
 
Bi.Mahiza alisema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni miaka 48 ya Muungano  shiriki kikamilifu katika sensa na mchakato wa mabadiliko ya katiba.
 
''Sherehe hizi zitapambwa na gwaride ,halaiki na ngoma kutoka mikoa mbalimbali Tanzania,ambapo pia aliwaomba  SUMATRA na wamiliki wa vyombo vya usafiri kuelekeza magari yao katika kuelekea uwanja wa Uhuru ili kurahisisha usafiri kwa wananchi wa Dar es Salaam"alisema.
 
Aliwaomba watanzania kudumisha Muungano kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho wache kusikia maneno ya mitaani kwa kuwa viongozi waliopita wasisi wetu waliomba tudumishe muungano huo.

MAGAZETI LEO

MELI YA MAGUFULI YAANZA KUZAMA


Did you Rihanna alizaliwa 1988

Rihanna born in 1988 in Barbados

Robyn Rihanna Fenty (born February 20, 1988), better known as simply Rihanna, is a Barbadian recording artist. Born inSaint Michael, Barbados, Rihanna moved to the United States at the age of 16 to pursue a recording career under the guidance of record producer Evan Rogers. She subsequently signed a contract with Def Jam Recordings after auditioning for then-label head Jay-Z.


Music
In 2005, Rihanna released her debut studio album, Music of the Sun, which peaked in the top ten of the Billboard 200 chart and features the Billboard Hot 100 hit single "Pon de Replay." Less than a year later, she released her second studio album, A Girl Like Me (2006), which peaked within the top five of the Billboard albums chart, and produced her first Hot 100 number one single, "SOS". Rihanna's third studio album, Good Girl Gone Bad (2007), spawned four chart-topping singles "Umbrella", "Take a Bow", "Disturbia" and "Don't Stop the Music", and was nominated for nine Grammy Awards, winning Best Rap/Sung Collaboration for "Umbrella," which features Jay-Z. Her fourth studio album Rated R, released in November 2009, produced the top 10 singles "Russian Roulette", "Hard" and "Rude Boy", which achieved the number-one spot on the Billboard Hot 100. Loud (2010), her fifth studio album, contains the number-one hits "Only Girl (In the World)", "What's My Name?" and "S&M" "We Found Love" was released in September 2011 as the lead single from her sixth studio album and has topped the charts in over ten countries. Talk That Talk, Rihanna's sixth album, is set to be released in November 2011.



MusicRihanna has sold more than 20 million albums and 60 million singles which makes her one of the best selling artists of all time. She is the youngest artist in Billboardcharts history to achieve eleven number-one singles on the Hot 100. As of March 2010, Rihanna has sold approximately 7.3 million album units and over 33.7 million digital singles in the United States. Billboard named Rihanna the Digital Songs Artist of the 2000s decade, and ranked her as the 17th Artist of the 2000s decade. She has received several accolades, including the 2007 World Music Awards for World's Best-Selling Pop Female Artist and Female Entertainer of the Year, and the 2011 Brit Award for Best International Female Solo Artist. She has also amassed a total of four Grammy Awards, four American Music Awards, and eighteenBillboard Music Awards. Rihanna has also been appointed the official ambassador of youth and culture for Barbados.
MusicInfluences
Rihanna has named Madonna as her idol and biggest influence, and said she wants to be the "black Madonna". She said: "I think that Madonna was a great inspiration for me, especially on my earlier work. If I had to examine her evolution through time, I think she reinvented her clothing style and music with success every single time. And at the same time remained a real force in entertainment in the whole world." Rihanna also cited Mariah Carey as her influence and idol. She said "I looked up to [Mariah] a lot and I still do. I admire her as an artist, and to [compete with her] was a moment I will never forget for the rest of my life. Of Janet Jackson, Rihanna has commented that "[s]he was one of the first female pop icons that I could relate to ... She was so vibrant, she had so much energy. She still has power. I’ve seen her on stage, and she can stand there for 20 minutes and have the whole arena scream at her. You have to love Janet." Beyoncé has been named as a major influence, citing that she was inspired to start her career after watching Knowles on television as part of a Destiny's Child performance. Her other musical influences include Bob Marley, (for whom she built a shrine in her Los Angeles home) Alicia Keys Whitney Houston, Destiny's Child, Celine Dion, Brandy and Gwen Stefani. Her friend and former Island Def Jam record label artist Fefe Dobson was someone that she admired and looked up to, having a fellow artist writing, singing, and performing the music she truly loves.
Singer







Rihanna's music contains strong influences of Caribbean music which include reggae and dancehall. The video for "Rude Boy" was inspired by her Caribbean roots. In an interview, she stated that while growing up in Barbados she grew up listening to reggae music and when she came to the United States she was exposed to many different types of music. During the Good Girl Gone Bad Tour, she did a cover to "Is This Love" which paid tribute to Marley; she would later do a cover song to Bob Marley & The Wailers' "Redemption Song". Rihanna commented that Marilyn Monroe and vintage clothing served for visual inspiration for the music video "Hate That I Love You" and "Rehab"; in contrast, the "dark, creepy" scenes of "Disturbia" have drawn comparison to Michael Jackson's Thriller. The music video ranked number five on the "Top Five Most Paranoid Music Videos" published by MTV Buzzworthy. Jon Bream of the Star Tribune commented "[i]n the tradition of Madonna and Janet Jackson, Rihanna has become the video vixen of the '00s ... Rihanna has perfected the pout, the long-legged strut and trend-setting hairdos that keep women and men alike checking her out on YouTube." George Epaminondas of InStyleconsiders Rihanna's music videos to be "cinematic" due to her "blend of lush island rhythms and swinging pop and ... mischievous sensuali



Kwa habari zaidi tembelea

wwb.reyqui.com/2011/11/robyn-rihanna

Tuesday, April 24, 2012

NDOLANGA, EL MAAMRY MARAIS WA HESHIMA TFF



 Ahmad  Ndolanga   kulia na Hamad  El Maamry kushoto
MWENYEVITI wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Said Hamad El Maamry na Muhiddin Ahmad Ndolanga wameteuliwa kuwa Marais wa heshima wa shirikisho hilo, katika Mkutano Mkuu wa TFF unaoendelea kwenye ukumbi wa NSSF Water Front, Dar es Salaam.

Habari kutoka ndani ya Mkutano huo, ambao utaendelea hadi kesho, zimesema kwamba viongozi hao wa zamani nchini wamepewa heshima hiyo na Wajumbe wa Mkutano Mkuu kutokana na mchango wao katika soka ya Tanzania, enzi zao wakiwa madarakani wakati TFF ikiitwa FAT (Chama cha Soka Tanzania).

Aidha, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wameambiwa kuwa Hati ya Uwanja wa Karume haishikiliwi na benki kutokana na deni la ziara ya timu ya taifa ya Brazil Juni 2012, zaidi ya Sh. Bilioni 3, kwani deni hilo lilidhaminiwa na Serikali.

Mkutano huo unatarajiwa kufungwa muda si mrefu katika siku yake ya kwanza leo, ili Wajumbe wakawahi kuangalia mechi ya timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro dhidi ya Sudan, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mkutano huo, utaendelea tena kesho katika siku ya mwisho na tarehe ya uchaguzi Mkuu, utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu, inatarajiwa kupangwa rasmi hiyo kesh

Monday, April 23, 2012

LULU ATINGA MAHAKAMANI YA KISUTU TENA

Mshtakiwa Elizabeth Michael |(17), ' Lulu'  (mwenye nguo nyekundu, )akiteremka ngazi huku akiwa chini ya ulinzi mkali baada ya kupandishwa Kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo Aprili 23.2012 ambapo kesi hiyo  ilikuja kwa ajili ya kutajwa.  Kwa mujibu wa Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Rita Tarimo  ni kuwa upelelezi bado haujakamilika na mtuhumiwa kurudishwa rumande hadi Mei 07 mwaka huu itakapotajwa tena.

Rais KIKWETE AKITOA HESIMA ZA MWISHO KWA BRIGEDIA JENERALI ADAMU ADAMU MWAKANJUKI APRILI 22


Friday, April 20, 2012

JARIBU KUPITIA MISTARI YA BIBLIA WEEK END


Zaburi 35:1 Ee Bwana utete nao wanaoteta nami Upigane nao wanaopigana nami.




 KUHUSU VILEVI KATIKA BIBLIA

Soma Waraka wa kwanza wa Petro, sura 4, kuanzia mstari wa kwanza mpaka wa mstari wa tano ( 1 Petro 04:01-05) inasomeka kama ifuatavyo:-
"
1 Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.
2 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika
ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.
5 Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

BUNGENI :WAZIRI MKUU AWEKWA REHANI




ZITTO ATAKA SAINI ZA WABUNGE 70 KUMNG'OA,MAWAZIRI WATANO WATAKIWA KUJIUZURU, FILIKUNJOMBE ADAI MKULO MWIZI

Na Waandishi wetu, Dodoma na Dar
BUNGE jana lilichafuka baada ya wabunge kuishambulia Serikali kwa kukumbatia ufisadi, huku baadhi yao wakiandaa mkakati wa kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Akifanya majumuisho ya hoja zilizotolewa na wabunge pamoja na mawaziri, Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC) Zitto Kabwe, alisema kuwa wanachohitaji kukamilisha mchakato huo ni kupata saini za wabunge 70.

Kwa sababu hiyo, akasema inabidi wabunge wenye uchungu na jinsi fedha za Serikali zinavyofujwa na watendaji mbalimbali wasaini kwenye karatasi hiyo ili hoja hiyo iwasilishwe bungeni Jumatatu.

Fukuto la kutaka Waziri Mkuu ajiuzulu lilianza katika kikao cha faragha cha  wabunge wa CCM kilichofanyika mchana, baada ya wabunge kutaka Serikali iwawajibishe mawaziri wezi vingine Pinda ajiuzulu.

Iwapo kura za kutokuwa na imani zitapigwa, huenda Pinda akalazimika kujiuzulu na matokeo yake Rais Jakaya Kikwete itambidi kulivunja Baraza la Mawaziri na kuunda jipya.

Zitto alisema mpango huo unapaswa kufanyika ili kuweka msingi wa uwajibikaji kwa viongozi wa nchi kwa sababu limekuwa ni tatizo sugu.

“Misingi ya uwajibikaji lazima iwekwe,” Zitto alisema akisisitiza kuwa ni moja ya jambo ambalo kama lingekuwa linatekelezwa nchini ama kuwekewa mkakati maalumu wa utekelezaji,Tanzania ingepiga hatua kimaendeleo.

Awali Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) amewaomba wabunge wote kuungana bila kujali itikadi za vyama vyao na kupiga kura ya kutokuwa na imani na Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu uendeshaji wa nchi.

Akichangia mjadala kuhusu taarifa hizo za kamati, Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Upinzani Bungeni, alisema wakati CAG, Ludovick Utouh amekuwa akitoa taarifa ya wizi wa kutisha, hakuna hatua zozote zilichochukuliwa na serikali.

Alisema tatizo linaloikabili nchi hivi sasa ni kuwa na mfumo wa utawala wa wizi ambao unalinda wezi na unaoadhibu watu wanaosema ukweli na kutoa mfano kuwa ukitaka ‘kushughulikiwa’ fuatilia wizi ndani ya halmashauri za wilaya.


“…wabunge tuache kulalamika tu- move a motion (tulete hoja) ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na serikali,”alisisitiza Lissu.



Filikunjombe
Awali, Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe jana alichachamaa bungeni na kumlipua Waziri wa Fedha, Mustapha Mkulo kwa madai kuwa ni mwongo na anaongoza kundi la mwaziri 19 wa Serikali aliodai, wanatafuna fedha za umma na kulifilisi taifa.

Filikunjombe alifikia hatua hiyo baada ya kutakiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu na Bunge William  Lukuvi kuomba mwangozo wa Spika, ukimtaka mbunge huyo kijana kuthibitisha madai aliyoyatoa wakati wa  mjadala wa kuchangia Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ambapo aliwashambulia mawaziri huku akiweka bayana kuwa ana ushahidi na majina 19 ya mawaziri,mchwa wanaolitafuna taifa.

"Mimi nina ushahidi wa mawaziri 19 na nikipata fursa nitamtaja mmoja kwa jina leo (jana) jioni," alisema.

Akizungumza kwa hisia, Filikunjombe alimtaja Mkulo akisema kuwa siyo mwaminifu na mwongo huku akionesha ripoti aliyodai imeanika madhambi yote ya Mkulo.

Alisema kuwa anashangaa kwanini tangu ripoti hiyo iwasilishwe, hakuna hata waziri mmoja aliyejiuzulu na kuongeza kuwa mawaziri hao wamekuwa na tabia ya kulindana.

“Nitamtaja Waziri mmoja ambaye anahusika na ubadhirifu huu. Waziri Mkulo siyo mwaminifu. Kila mbunge anayoripoti hii inayoeleza ubadhirifu huu,” alisema Filikunjombe na kuongeza;
“Alitaka kuifuta CHC, waheshimiwa wabunge tukapigana humu Bungeni tukashinda, …alipoona Mkurugenzi wake anamfuatilia, alimsimamisha kazi na kuisimamisha kazi bodi ya shirika hilo. Waziri Mkulo ni mwongo!”

Alitoa mfano wa jinsi fedha za Serikali zinavyopotea akiitaja Taasisi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwamba licha ya fedha nyingi kupelekwa huko, zimekuwa zikiliwa na wakuu wa vyuo.
Alimtaja Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki  cha Mkwawa akisema kuwa anahusika moja kwa moja na wizi wa fedha hizo.

Filikunjombe pia alimtaja Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami kuwa amekuwa akilinda uozo wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa maslahi yake binafsi.

“Kuhusu hili la Shirika la Viwango (TBS) ambalo halina viwango….Waziri Chami amekuwa akilinda TBS kwa nguvu zake zote… najua ulinzi huo siyo wa bure, mnakumbatia mmoja. TBS hawafanyi ukaguzi wowote, kuna blueband mbovu, vyakula vibovu, mafuta ya ndege feki, matairi feki ndiyo maana hata ndege ilianguka kule. Maisha ya Watanzania yako hatarini” alisema Filikunjombe.

Huku akimkazia macho Waziri Mkuu, Filikunjombe alisema kuwa baadhi ya mawaziri wake si waaminifu na kuongeza kuwa nchi hii sio ya CCM wala hivyo haipaswi kusubiri hadi wapinzani waseme au waandamane.


Wabunge wa CCM
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Pinda jana alijikuta katika wakati mgumu baada ya wabunge wa CCM kumtaka ama ajiuzulu au awafukuze kazi mawaziri wake watano wanaohusishwa na tuhuma mbalimbali zikiwamo za kushindwa kuwajibika na kuruhusu ufisadi wa kutisha kufanyika.

Huo utakuwa ndio mtihani wa kwanza mkubwa kuwahi kumkumbua Waziri Mkuu huyo tangu ashike wadhifa huo Februari 2008,  huku akiwa na kumbukumbu ya mtangulizi wake, Edward Lowassa aliyelazimika kujiuzulu kwa shinikizo la wabunge.

Shinikizo la Waziri Mkuu kutakiwa ama kujiuzulu ama kuwatosa mawaziri wake hao lilianzia ndani ya Bunge na baadaye kuhamia katika kikao cha faragha cha Wabunge wa CCM kilichoitishwa kujaribu kupunguza makali ya Wabunge hao dhidi ya serikali.

Mawaziri waliomponza Waziri Mkuu Pinda ni pamoja na Waziri wa Fedha, Mkulo, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (Tamisemi), George Mkuchika, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami na Naibu wake, Lazaro Nyalandu.

Hasira ya Wabunge hao ilitokana na ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na taarifa za wenyeviti wa kamati tatu za kudumu, zote zikionyesha wizi na ufisadi wa mabilioni ya shilingi katika serikali kuu, mashirika ya umma na Halmashauri mbalimbali za wilaya na majiji.

Taarifa zilizovuja kutoka ndani ya kikao hicho kilichoanza saa 7.10 mchana hadi saa 11:08 mchana zilieleza wabunge walimshambulia waziwazi Waziri Mkuu Pinda kuwa amekuwa na kigugumizi kisicho cha kawaida na mzito wa kuchukua maamuzi dhidi ya wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali kutoka ndani ya kikao hicho, wabunge hao walimtuhumu Waziri Mkuu kuwa amekuwa akimshauri vibaya rais na hivyo kushindwa kuwafukuza mawaziri hao wanaonekana kuwa ni mzigo kwa Serikali na kuifanya iboronge katika utendaji.

“Kwa ujumla Pinda hana hatia, lakini kikubwa kinachomfanya asulubiwe ni kitendo chake cha kuwa na kigugumizi kwa kushindwa kufikisha majibu sahihi ya wabunge kwa rais na kutufanya tuendelee kuwa na hii mizigo,’’kilisema chanzo hicho kimoja cha kuaminika.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, wabunge waliokuwa msumari wa moto kwa serikali ni pamoja na Livingston Lusinde, Zainab Kawawa, Godfrey Zambi,Michael Laizer pamoja na Peter Serukamba ambao kila mmoja alitoboa hadharani kuwa Serikali imeoza.

Zainabu aliwaeleza wabunge kuwa kwa hali ilikofikia sasa,kama waasisi wa Taifa hili wangefufuka na kupata hata dakika moja tu ya na kushuhudia madudu yanayofanyika,wangeamua kujiondoa tena kutoka ndani ya CCM na tena wangeondoka kutokana na aibu hizi.
“Kwa ujumla ninyi wazee hamfai, tena hamfai kabisa mnakotupeleka ni kubaya kulikooza hebu tuondoleeni aibu hiyo,’’alisema Kawawa.

Kwa upande wake Lusinde alimueleza Waziri Mkuu Pinda kuwa anafanya kila namna ya kuhakikisha kuwa kila kitakacholetwa katika kipindi cha bajeti kinakwamishwa kutokana na yeye kuwa na zaidi ya vijiji 71, lakini havina maji hata kidogo huku baadhi ya mawaziri wakibeba kila kitu cha nchi hii na kupeleka katika majimbo yao.

Lusinde alisema yuko tayari kujiuzulu ubunge pamoja na nafasi zake ndani ya chama kwani hakuna faida ya yeye kuwa mbunge huku mawaziri wakiendelea kumdanganya.

Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi alimtaka Waziri Mkuu kufikisha kwa Rais Jakaya Kikwete mara moja hoja ya kuwafukuza Mawaziri mzigo na kusema kuwa kama hatafanya hivyo bunge halitakalika.

“Kikubwa unachotakiwa kumfikishia rais ni kuwa hawa mawaziri ni mzigo, wameoza tafadhali sana bila ya hivyo bunge halitakalika hapa tunakwambia maana hata akibadilisha Waziri Mkuu lakini bila ya hawa jamaa kuondoka ni sawa na kazi bure,’’alisema Zambi.

Mbunge wa Longido, Michael Lekule Laizer alimtaka Pinda kufikisha ombi lake kwa rais na kumueleza kuwa kama ameshindwa kuwafukuza mawaziri hao basi ni lazima avunje Serikali na nchi irudi katika uchaguzi.
Lazier alisema mahali ilipofikia sasa ni pabaya ambapo kila mmoja anatakiwa kubeba msalaba wake mwenyewe na kufa nao vinginevyo shimo hilo litawatumbukiza wengi hata wale ambao hawakuhusika.
Chanzo kingine cha habari kilisema wabunge hao walifikia maazimio ya kumpa muda Waziri Mkuu kwenda kuwasiliana na Rais juu ya kuwawajibisha mawaziri hao na kama hatafanya hivyo watapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali katika Bunge lijalo.

Ole Sendeka azomewa
Katika kikao hicho wabunge walimzomea Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole-Sendeka baada ya kusimama na kuonyesha wazi kuwa anawatetea mawaziri hao walioonekana kuchafua hali ya hewa.

Inadaiwa Ole Sendeka aliwataka wabunge wenzake kupunguza hasira na kuwasamehe mawaziri akisema kuwa nao ni binadamu ambao kwa vyovyote lazima wawe na mapungufu.

Kauli hiyo iliufanya ukumbi huo wa Msekwa kulipuka kwa kumzomea kabla ya Mbunge wa Kigoma, Mjini Peter Serukamba kumueleza mbunge huyo kuwa “ huna sera kwa leo kaa chini”.

Wakati hayo yote yakitokea, hakuna Waziri aliyepewa nafasi ya kueleza jambo lolote au kujitetea kwani hata Waziri Mkuu alijibu kwa ufupi kuwa wameyasikia na wanakenda kuyafanyia kazi.

Mbowe
Naye kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alionyesha kushangazwa na kutokuwepo kwa wabunge wengi wa CCM akisema kuwa wamekwenda kwenye mkutano na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili kuinusuru Serikali ya CCM.

Mbowe aliyekuwa wa kwanza kuchangia katika kipindi cha jioni, alisema atahamasisha wananchi kote nchini kuandamana ili kuiondoa madarakani Serikali iliyoshindwa kuwajibika.

“Katika historia ya Bunge hili tangu lilipoanza kuonyeshwa moja kwa moja, sijawahi kuona wabunge wakitoka bungeni ili kuinusuru Serikali na kuacha watu sita tu wa kukaba nafasi,” alisema Mbowe.
Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa Chadema, alisema kuwa licha ya wabunge wa upinzani ukupiga kelele kuhusu ubadhirifu serikalini bado hawasikilizwi.

“Wananchi wajue kwamba wabunge wa upinzani hatusikilizwi bungeni, lakini tukiandamana ndiyo tutasikilizwa. Kama wabunge na mawaziri wa CCM wameondoka bungeni, basi watupishe na Ikulu na ofisi nyingine tuwaonyeshe nanma ya kufanya kazi,” alisema Mbowe.

Wabunge wengine
Naye Mbunge wa Kasulu Mjini Moses Machali aliitaka Serikali kuchukua hatua kali kwa wote waliohusika na ubadhirifu huo ikiwa ni pamoja na kuwanyonga,
“Unaweza kuwadanganya baadhi ya watu kwa wote na unaweza kuwadanganya watu wote kwa wakati fulani lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati wote. Mambo haya yamesema mno…… Waliosababisha haya yote wakamatwe na wanyongwe hadharani ili iwe fundisho kwa wengine watakaohusika” alisema Machali.

Machali pia alimlaumu Waziri Lukuvi kwa kile alichosema kuwa ni kuchakachua kauli za wabunge.
Kwa upande wake Mbunge wa Musoma mjini Vincent Nyerere alikumbushia swali alilomuuliza juzi Waziri wa Viwanda na Biashara Dk Chami kuhusu ukaguzi wa magari akikosoa kuwa waziri huyo hakusema kweli.
Alitaja kampuni alizoziita kuwa za kitapeli akisema kuwa zimekuwa zikijifanya kukagua magari wakati si kweli.

“Septemba 25, 2007 kuna wajanja walikutana pale hoteli ya Movenpick na kuanzisha kampuni za ukaguzi wa magari ili zionekane kuwa ni kampuni za nje. Hakuna magari yanayokaguliwa kama alivyosema Waziri” alisema Nyerere.

Aliongeza kuwa tangu ukaguzi huo feki ulipoanzishwa kampuni hizo zimepata dola za Marekani 18 milioni (zaidi ya Sh 23 bilioni) huku Serikali ikiambulia dola milioni mbili tu.


Mapema, wakati akichangia mjadala  wa taarifa za kamati tatu za kudumu za Bunge, Dk. Chami alisema wizara yake imetekeleza maazimio yote ya kamati kuhusiana na kashfa ya ufisadi katika Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Katika mchango wake, Dk. Chami aliliambia Bunge kuwa yupo tayari kujiuzulu wadhifa huo endapo itathibitika kuwa yeye au ndugu, rafiki zake wa karibu, wana maslahi yoyote katika kashfa hiyo ya TBS ya kuyapa kazi makampuni bandia  ya ukaguzi wa mizigo nje ya nchi.

“Mheshimiwa Naibu Spika, inaonekana kumejengeka hisia bungeni kuwa tunamlinda Ekelege kama mtu ana uthibitisho nina maslahi katika hili au ndugu yangu niko tayari kuuweka rehani uwaziri wangu…niko tayari kujiuzulu,”alisema.

Dk. Chami alijitetea kuhusu taarifa ya maalumu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwamba ndiyo kwanza ilikuwa imemfikia juzi jioni, hivyo akawaomba wabunge waamini kuwa wizara yake ilikuwa haijapatiwa matokeo ya taarifa hiyo.

Mapema, Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi (CCM) alipendekeza kuwa kwa halmashauri ambazo zimekuwa na tuhuma nzito za ufisadi, wakurugenzi wake wasimamishwe kazi wakati uchunguzi wa tuhuma hizo ukiendelea.

Naye Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), alilitaka Bunge kutumia mamlaka yake ya kikatiba kuchukua hatua kwa vile kama ni kusema basi wametumia asilimia 70 ya muda wao kusema na sasa wanahitaji kuchukua hatua kwani hakuna mabadiliko.
 
Hali kadhalika, Mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Maselle (CCM) alitaka kufumuliwa kwa TBS akisema inasikitisha kuwa bidhaa feki zinaendelea kuzagaa nchini na mbaya zaidi ni kuingizwa nchini kwa maziwa feki ya watoto jambo ambalo ni la hatari zaidi.

Mbunge wa Viti Maalumu, Christowaja Mtinda(Chadema) alishangaa jina lake kuorodheshwa kuwa ni mtumishi wa Chuo Kikuu Huria nchini (OUT) wakati si mtumishi wa chuo hicho na kuhoji mshahara huo ni nani anayelipwa.

SOURCE MWANANCHI

Thursday, April 19, 2012

WAZIRI MKUU MIZENGO AKIZUNGUMZA NA MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI JOSHUA NASSARI NJE YA UKUMBI WA BUNGE


JAMANI TUMSADIE WASTARA


Nakumbuka rafiki yangu Gerald Hando aliniambia Dina ukisikiliza sana matatizo ya watu unaweza ukaogopa maisha.Yaani leo nimealia na nimehuzunika sana nilipokutana na Wastara na kunipa hadithi nzima ya kinachomkabili sasa.Na mpaka naandika hapa bado namfikiria sana.Ni mwanamke aliyepitia mengi na anendelea kupitia mitihani mingi akiongea analia kiasi cha kunifanya hata mimi nilie.Kweli binadamu hatujafa hatujaumbika tumshukuru Mungu kwa kila jambo unaweza kudhani wewe una mitihani hapa duniani kumbe kuna aliyekuzidi.
Najua nilikuahidi kuwa nitaruka leo na Wastara live katika leo tena ila nilichofanya nimerekodi kipindi kizima ambacho kitaruka hivi karibuni.Huyu mwanamke anahitaji msaada sana wa mumewe kutibiwa mwezi ujao anatakiwa kusafiri kwenda India kwa hayo matibabu ambayo yanaweza kugharimu zaidi ya ml 25 hela ambayo hata robo yake hawana.Nitakuomba sana mtanzania ushirikiane nami na hii familia hata kama hatutafikia pesa yote angalau ifike nusu.Hapa nimeshaanza kufanya mazungumzo na watu kadhaa ninao wajue ili tuhamasishane kuchangia haya matibabu.Wasanii tunaowaona kwenye movie wakiendesha magari ya kifahari na majumba yale sio maisha yao halisi hata kidogo ni watu na shida zao.
Kuna ac namba nitaitoa pamoja na tigo pesa ili kwa unaeweza kuchangia kwa huko.


 Kwa habari zaidi soma Dina Marios blog

MAMBA NYAMA YAKE TAMU

 
Nyama ya mamba itamuu nyama ya mamba itamuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu...kwa ugali,itamu...kwa ubwabwa itamuuuuuuuuuuuuu...kwa pilau itamuuuuuu