Tuesday, July 24, 2012

Waziri ajiuzulu baada ya ajali ya meli Zanzibar





Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano wa Serikali ya Zanzibar Hamad Masoud Hamad amejiuzulu wadhifa wake, jana kufuatia ajali ya kuzama kwa meli ya MV Skagit iliotokea Julai 18, 2012.

Na Victor Robert Wile
 

 Hatuwa hiyo imefikiwa baada ya rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Ali Mohammed Shein amekubali ombi la Waziri Hamad Masoud kujiuzulu.


Kufuatia kujiuzulu kwa waziri huyo, Dk. Shein amemteua mwakilishi wa Jimbo la Ziwani kupitia Chama cha Wananchi, CUF, Bwana Rashid Seif Suleiman kuchukua nafasi hiyo.

Katika hatua nyingine makamu wa pili wa rais wa serikali ya Zanzibar balozi Seif ali idd ametangaza kusitisha safari zote za meli ya MV Karama ambayo inamilikiwa na Kampuni ya Sigal kufanya safari zake kati ya Zanzibar na Dar baada ya kubainika kwamba inauwezo wa kusafiri umbali wa kilometa saba pekee.

Wakati huo huo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Ali Mohammed Shein ameunda Tume ya kuchunguza ajali ya kuzama kwa meli ya MV Skagit.
 

Thursday, July 19, 2012

Taarifa ya meli kuzama Zanzibara


Jumatano, July 18, 2012

Taarifa ya Serikali Meli iliyozama 


MAAFA YA KUZAMA KWA MELI ZANZIBAR

Meli ya Mv. Star Gate imezama karibu na Kisiwa cha Chumbe ambapo watu 12 wamefariki hadi muda huu na wengine kadhaa wamejeruhiwa.

Akitoa taarifa fupi kwa waandishi wa habari,Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Mwinyihaji Makame Mwadini alisema taarifa za kuzama kwa meli hiyo ilitolewa na Boti iendayo kasi ya Kilimanjaro III iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Zanzibar ndipo ilipoiona meli hiyo ikizama.

“Tulipata taarifa kutoka Boti ya abiria ya Kilimanjaro III saa 7:50 mchana waliporipoti kuona meli ikizama karibu na Kisiwa cha Chumbe” Alisema Waziri Mwinyihaji.

Waziri huyo alisema Meli hiyo imezama maili sita kuelekea Kisiwa cha Yasin Kusini mwa Kisiwa cha Chumbe kilichopo Unguja maili kadhaa kutoka Bandari ya Malindi.

Waziri Mwinyihaji alisema idadi ya abiria walikuwa 250 ambao ni watu wazima, watoto 31 na mabaharia 6. “Tumepeleka waokoaji, kuna boti tano zipo eneo la tukio kushirikiana na waokoaji wengine” Alisema Waziri Mwinyihaji.

Alisema maiti zote zitapelekwa viwanja vya Maisara Zanzibar kwa ajili ya ndugu na jamaa kuzitambua maiti za ndugu zao ambapo majeruhiwa wote watatibiwa Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.

Katika Bandari ya Malindi mwandishi wetu ameshuhudia maiti kadhaa zikiwemo za watoto zikishushwa, Miongoni mwa abiria waliookolewa ni raia 13 wa Mataifa mbalimbali ya nje huku raia mmoja ambaye hakuweza kutambuliwa utaifa wake amepoteza maisha.

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd alifika eneo la Bandari ya Malindi Zanzibar pamoja viongozi wengine akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, Mawaziri na baadhi ya Wajumbe a Baraza la Wawakilishi walikuwepo kutoa msaada unaohitajika.

Katika eneo la pembezoni mwa bandari ya Malindi, makundi ya wananchi yalikuwa yamekusanyika wakisubiri taarifa za tukio hilo tangu saa 8:30 mchana.

Vikosi vya ulinzi na usalama, msalaba mwekundu na watoaji wengine wa misaada ya dharura walifika kwa haraka eneo la tukio.

Hadi sasa kazi ya uokoaji inaendelea karibu na Kisiwa cha Yasin ilikozama meli hiyo.

Meli ya Mv. Star Gate inamilikiwa na kampuni ya kizalendo ya Sea Gull Sea Transport Ltd ambayo mwaka 2009 Meli yake nyengine ya Mv. Fatih ilipinduka na kuzama katika Bandari ya Malindi Zanzibar na kua watu sita.

Mwaka jana Zanzibar ilikumbwa na maafa baada ya Meli ya Mv. Spice Islanders kuzama katika bahari ya Hindi eneo la Nungwi katika Kisiwa cha Unguja ikielekea Kisiwani Pemba ambapo taarifa rasmi ya Serikali ilisema watu 197 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa.

MELI YA SKAGIT YAZAMA

Meli ya Skagit inayomilikiwa na  Kampuni ya Seagull imezama Maeneo ya Chumbe


Meli ya Mv Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar kuelekea Zanzibar imezama majira ya saa nane mchane hivi leo katika maeneo Pungume na Chumbe baada ya kukumbwa na upepo mkali.

Meli hiyo inayosadikiwa kuwa na abiria 250 inasemekana imepindukia upande mmoja na huku abiria wengi wakiweza kuokolewa kutokana na jitihada mbali mbali kupitia vile vile msaada wa boti za Mv Kilimanjaro, Tug ya Bandari na vyombo vyengine

UKIMWI

Dawa mpya kwa wagonjwa wa Ukimwi

Baadhi ya dawa za kukabiliana na makali ya Ukimwi
Huenda wagonjwa wa Ukimwi wakanufaika na dawa mpya ambayo itawawezesha kutumia tembe moja kwa siku. Hii ni kwa mujibu wa utafiti mpya nchini Marekani.

Jarida la Afya Lancet limesema tembe hiyo inajumlisha dawa zote nne zinazokabiliana na makali ya ukimwi na kwamba ni salama.Utafiti unasema hii itawarahisishia wagonjwa katika kuhakikisha wanafuata maagizo ya madaktari wao.

Ukimwi hauna tiba lakini watafiti wameweza kutoa dawa za kukabiliana na maradhi nyemela.

Watafiti pamoja na kampuni za dawa wamechanganya dawa nne na kutengeneza tembe moja ili kurahisisha utumizi wa dawa hiyo miongoni mwa wagonjwa.

Tembe inayofanyiwa majaribio na ambayo imechanganywa dawa nne inauwezo wa kudhibiti virusi vya HIV kuongezeka mwilini.

Paul Sax mtafiti mkuum katika Hospitali ya Wanawake ya Brigham huko Boston,Massachussetts ambaye pia ni mwanazuo wa ziada wa taasisi ya afya ya Harvard ameelezea umuhimu wa tembe hii kwa kuimarisha afya ya wagonjwa.

Dk. Sax ameongoza utafiti huu ambapo pia wamefanyia majaribio tembe hii kwa wagonjwa 700 na kusema inafanya kazi, japo kulitokea matatizo ya figo miongoni mwa waliotumia.

Licha ya mafanikio ya sasa watafiti wanasema raia wengi hawafahamu hali zao ambapo wameendelea kuishi na maambukizi bila kujua.HABARI KWA HISANI YA  zanzibarwebsite.com

http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2012/06/120629_hiv_quad.shtml

MAPISHI YA CHAPATI

activechef.blogspot
JIFUNZE KUTENGENEZA CHAPATI YA AINA YAKE KWA KUTUMIA NAFAKA ZA AINA 15 PAMOJA NA MCHELE WA BROWN, NI TAMU SANA NA FAMILIA ITAFURAHIA SANA

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI
     FUTANA na    activechef.blogspot.com




















Wednesday, July 18, 2012

Kova

Kova: Sitaki malumbano *Adai sakata la Dkt. Ulimboka liachiwe mahakama *Asema ni kinyume cha katiba kujadili jambo hilo



Na Stella Aron

KAMANDA wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema jeshi hilo haliwezi kuingia kwenye mtego wa malumbano na taasisi za dini ambazo zinaongozwa na Wakristo, Waislamu au madhehebu mengine.

Kamanda Kova aliyasema hayo Dar es Salam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kauli iliyotolewa na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufua na Uzima, Josephat Gwajima.

Katika mahubili yake yaliyofanyika kanisani hapo Dar es Salaam juzi, Mchungaji Gwajima alikanusha taarifa zilizotolewa na Jeshi la Polisi kuwa, mtuhumiwa anayedaiwa kumteka nyara, Dkt. Steven Ulimboka, alikwenda kwenye katika hilo kufanya toba.

“Hivi sasa sakata hili halizungumziki kwa kuwa mtuhumiwa tayari amefikishwa Mahakamani, kesi yake ni PI 5/2012 na yupo rumande gerezani akikabiliwa na shtaka la utekaji nyaraka na kujaribu kuua.

Kamanda Kova aliongeza kuwa, sakata la Dkt. Ulimboka (Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini) na kukamatwa kwa mtuhumiwa Bw. Joshua Gitu Mhindi, limefungwa kwani kuendelea kulizungumza ni kuingilia uhuru wa mahakama.

“Ni kinyume cha Katiba ya Tanzania kujadili jambo ambalo liko Mahakamani kama ilivyo katika shauri hili, kama tukiendelea kulizungumzia, Mahakama itashindwa kuendelea na kesi.

“Namheshimu sana Mchungaji Gwajima, nisingependa kujibu hoja zote alizotoa, kazi ya Jeshi la Polisi ni kufanya doria za mwili, mitaa, vijiji na viongozi wa dini wanafanya doria za kiroho ambapo utii wa sheria bila shuruti ni kazi ya polisi, utii ni thawabu kwa Waislamu na baraka za utii kwa Wakristo,” alisema Kamanda Kova.

Alisema polisi wana wajibu wa kudumisha amani ili waumini wa dini zote wasali kwa uhuru bila hofu hivyo jeshi hilo halipo tayari kuendelea na malumbano hayo.

“Tunawaomba wananchi waendelee kuliamini Jeshi la Polisi na kutupa ushirikino kwa kutoa taarifa za uhalifu kwani kumekuwa na uvumi unaosababisha upelelezi kuchelewa,” alisema na kuongeza kuwa, kuna uvumi unaondelea kuhusu suala la utekwaji nyara Dkt. Ulimboka ambao unaweza kuchelewa upelelezi.

Kamanda Kova alisema, jeshi hilo lina uhakika na ushahidi wa mtuhumiwa Bw. Mhindi, kutokana na maelezo aliyotoa polisi hivyo na wasingependa kuyaeleza kwani wataingilia uhuru wa mahakama.

Kuhusu madai kuwa mtuhumiwa ni kichaa au mwendawazimu, Kamanda Kova alisema, mwenye uwezo kisheria wa kuthibitisha madai hayo ni daktari pekee.

“Hata kichaa anamilikiwa na sheria, kama akifanya makosa ya jinai anashughulikiwa kama mhalifu ambaye kama atafanya kosa la jinai, hawezi kuachwa hivi hivi,” alisema.

Juzi Mchungaji Gwajima, alilitupia lawama Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kudai kuwa, mtuhimiwa Bw. Mhindi hakufika katika kanisa lake kufanya sala ya toba na kudai kuwa, mtuhumiwa huyo ni kichaa.