Tuesday, May 8, 2012

LULU MAHAKAMANI TENA 3


Msanii wa filamu za maigizo nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, leo amepandishwa tena kizimbani mara ya tatu katika kesi ya mauaji ya Kanumba inayomkabili ambapo mawakili wanaomtetea wakiongozwa na Kennedy Fungamtama waliwasilisha ombi la kurekebisha umri wa mshitakiwa huyo kuwa miaka 17 na si 18 kama ilivyowasilishwa mahakamani hapo.


Fungamtama na jopo lake walisema mteja wao ni mtoto mdogo hivyo kesi hiyo ipelekwe mahakama ya watoto na kuwasilisha cheti kinachoonesha ana umri wa miaka 17. 



Upande wa mashitaka umetupilia mbali ombi hilo na kudai cheti kilichowasilishwa kina mapungufu kadhaa likiwemo jina la Dyana ambalo halijawahi kusikika likitumiwa na mshitakiwa huyo.

MKAPA MAHAKANI KISUTU




•  Waliotemwa uwaziri wamsusa


na Mwandishi wetu

RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, jana aliikaanga serikali ya Jakaya Kikwete mahakamani akidai kuwa hakuna ubadhirifu wowote uliofanywa na aliyekuwa Balozi wa Italia, Prof. Costa Mahalu, katika ununuzi wa jengo la ubalozi nchini humo.
Akiongozwa na wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa, baada ya kuapa alieleza kuwa kati ya mwaka 1995-2005 akiwa Rais alifahamu ununuzi wa jengo la ubalozi nchini Italia kwa euro 3,098,741.40, na kuwa hata aliyekuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ni Rais wa sasa, Jakaya Kikwete alikubaliana na ununuzi huo.
Mkapa ambaye ni shahidi wa Mahalu katika kesi hiyo alisema mwaka 2003 yeye ndiye aliyekwenda mjini Rome-Italia kulizindua jengo hilo la kisasa, Profesa Mahalu akiwa balozi.
“Serikali yangu iliarifiwa bei na taratibu za kulinunua na mimi kama Rais wa nchi nilitaarifiwa kuwa muuzaji alitaka malipo yafanywe mara mbili tofauti katika akanti zake …na mimi kwa niaba ya serikali yangu nikatoa idhini linunuliwe kwa mtindo huo nilioutaja hapo juu,” alidai Rais Mkapa.
Mahalu anatuhumiwa kuidhinisha kwa niaba ya serikali ununua wa jengo la ubalozi kwa thamani ya euro milioni 3 kwa njia ya mikataba miwili na kwa akaunti mbili.
Mawakili: Wewe au serikali ya awamu ya tatu iliwahi kupokea malalamiko toka serikali ya Italia kuwa ubalozi wetu nchini humo ulivunja sheria kuhusu mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa: Hapana, sijawahi kupokea malalamiko.
Mawakili: Ukiwa Rais hujawahi kupokea malalamiko kuwa fedha za serikali yetu zilizotumwa kwa ajili ya kumlipa muuzaji wa jengo hilo kuwa hazijamfikia?
Mkapa: Hadi leo hii natoa ushahidi hapa mahakamani sijawahi kupokea malalamiko ya aina hiyo.
Mawakili: Uliwahi kupata malalamiko toka kwa CAG, Wizara ya Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi, Waziri wa Mambo ya Nje, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala Ofisi ya DPP kuhusu ubadhirifu wa ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa: Sijawahi kupata.
Mawakili: Nini ufahamu wako kuhusu utumishi wa Profesa Mahalu?
Mkapa: Namfahamu kama msomi mzuri, mchapakazi, muadilifu na kiongozi anayetenda haki.
Mawakili: Mawasiliano kati ya serikali na balozi yanafanyika kwa njia zipi?
Mkapa: Balozi anaweza kuwasiliana na serikali yake kwa njia ya barua kwa Wizara ya Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi, Rais au kwa njia ya mdomo. Na mawasiliano siyo lazima yafanyike kwa njia ya maandishi tu kwa sababu maelekezo mengine ambayo anapewa balozi na serikali yake ni ya siri kwa maslahi ya taifa hivyo anaweza kuitwa nyumbani na kupatiwa maagizo hayo kwa njia ya mdomo.
Mawakili: Kwa wadhifa wako ule wa urais, kabla ya kwenda kuzindua jengo hilo Januari 23, 2003, hukuwahi kupokea taarifa toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na DPP za kukukataza usiende kuzindua jengo hilo kwa sababu kulikuwa na harufu za ubadhirifu wa fedha za umma?
Mkapa: Ofisi hizo hazikuwahi kunipatia taarifa hizo.
Yafuatayo ni mahojiano baina ya mawakili wa serikali
Mawakili: Hebu ieleze mahakama ni kwa nini bei za jengo zinatofautiana maana risiti za manunuzi zinaonyesha lilinuliwa kwa euro milioni 3 na hansard ya Bunge iliyosomwa na Kikwete bungeni mwaka 2004 inasema ilinuliwa kwa shilingi bilioni 2.9?
Mkapa: Kazi yangu siyo kufanya uthamini wa fedha za kigeni kwamba wakati huo hizo euro milioni 3 zilikuwa na thamani gani kwa fedha Tanzania (kicheka).
Mawakili: Nani aliagiza upelelezi wa manunuzi ya jengo la Italia ufanyike?
Mkapa: Sijui.
Mawakili: Uchunguzi wa jengo hilo ulifanyika wakati wewe ukiwa madarakani?
Mkapa: Sijui, nilikuja kuona Balozi Mahalu kashtakiwa mwaka 2007 nikiwa tayari nimestaafu. Nilithibitisha taarifa hizo kupitia vyombo vya habari kuwa ameshtakiwa.
Mawakili: Nani alikupa taarifa za muuzaji wa jengo hilo anataka kulipwa kwa mtindo huo wa akaunti mbili?
Mkapa: Ni Mahalu na alinipa taarifa kwa mdomo na alikuwa ameandaa ripoti juu ya ununuzi na akawa anaomba ridhaa ya serikali kabla ya kulinunua.
Mawakili: Ulisema hukuweza kuzuia ununuzi wa jengo, je ulikuwa na madaraka ya kuweza kuzuia lisinunuliwe?
Mkapa: Eh! Mimi ndiye nilikuwa Rais wa nchi; nilikuwa na madaraka hayo na badala yake fedha hizo zingeelekezwa kwenye mahitaji mengine ila kwa sababu nilikuwa ninajua umuhimu na faida ya nchi kununua jengo lile ndiyo maana nikaridhia kwa mdomo linunuliwe.
Wakili: Ulitoa maelekezo kwa nani?
Mkapa: Nilitoa maelekezo kwa njia ya mdomo kwa watendaji na maagizo hayo yalipaswa yatekelezwe na Wizara ya Mambo ya Nje na ilikuwa jukumu la Mahalu kuieleza wizara hiyo na ubalozi utekeleze maagizo yangu.
Wakili: Kwa hiyo unaieleza mahakama kuwa Wizara ya Mambo ya Nje, ilituma malipo kwa mtindo wa akaunti mbili tofauti?
Mkapa: Inahusu nini sasa? Mimi nilitoa maagizo, hivyo lilikuwa ni jukumu la Balozi Mahalu kuieleza wizara yake. Sasa suala la hayo makaratasi ya kufanya mchakato wa kulinunua, mimi kama Rais siwezi kuingilia. Watendaji walipaswa watekeleze.
Mawakili: Utajisikiaje tukikwambia kuwa yule muuzaji aliyetuuzia jengo kwa mtindo wa akaunti mbili alikuwa akikwepa kodi kwa serikali ya Italia?
Mkapa: Aaah! Mi’ sioni tatizo; kikubwa hapa Tanzania tumepata jengo, Alhamdulilah (kicheko).
Mawakili: Utajisikiaje ukisikia Mahalu alitumia zile euro milioni 3 kwa matumizi yake binafsi?
Mkapa: Nitashangaa sana. Pia wewe wakili wa serikali ndiyo nitakushangaa zaidi kwani hansard ya Bunge iliyosomwa na Kikwete bungeni imetamka bayana kuwa serikali ilimlipa muuzaji wa jengo na kwamba taratibu na sheria ya manunuzi ya umma zilifuatwa na hadi sasa huyo muuzaji hajawahi kulalamika kuwa hajalipwa fedha zake.
Rais Mkapa aliingia mahakamani hapo saa 3:45 asubuhi akiwa katika gari aina VX lenye namba T 745 BQE akiongozwa na walinzi wake.
Maafisa toka Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) walionekana kuingia katika viwanja vya mahakama hiyo kabla ya kiongozi huyo kuwasili.
Hakimu Mkuu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Ilvin Mugeta, aliahirisha kesi hiyo hadi leo ambapo mshtakiwa wa pili aliyekuwa Meneja Utumishi na Utawala wa Ubalozi huo, Grace ataanza kujitetea
www.freemedia.co.tz

Friday, May 4, 2012

KIKWETE APANGUA BARAZA LA MAWAZIRI SURA MPYA ZATAWALA


Friday, May 04, 2012


Baraza La Mawaziri

Wassira anaendelea na nafasi yake
Celina Kombani kabadilishiwa Wizara
Nagu anaendelea
Lukuvi anaendelea na wizara yake
Ghasia kabadilishiwa Wizara
Sitta anaendelea na Afrika Mashariki
Nahodha anahamia Wizara ya Ulinzi
Magufuli anaendelea na nafasi yake
Hussein Mwinyi kahamishiwa Afya
Kawambwa anaendelea na ElimuS
Membe anaendelea na Mambo ya Nje
Chikawe anarudi Katiba na Sheria
Sofia Simba na nafasi yake
Nchimbi - Mambo ya ndani
Mathayo David anaendelea
Kabaka anaendelea na nafasi yake
Mbalawa anaendelea na nafasi yake
Tibaijuka anaendelea na nafasi yake
Chizza anakuwa Waziri wa Kilimo chakula na ushirika
Maghembe - Maji
Mwakyembe anakuwa Waziri wa Uchukuzi

Mkuchika- Utawala bora
Samia suluhu – Muungano
Huviza – Mazingira
Mery nagu – Uwekezaji
Lukuvi – Uratibu na sera
Hawa gasia – TAMISEMI
Samweli sita- East Africa
Shamsi nahodha- ulinzi
Magufuli- ujenzi
Hussen mwinyi- Afya na ustawi
Shukuru kawambwa- Elimu na Mafunzo
Sofia – Maendeleo ya jamii
Membe – Nje
Mathia Chikawe – katiba na Sheria
Emmanuel Nchimbi – Ndani
David Matayo – Mifugo
Kabaka – Kazi na Ajira
Prof marawa- Mawasiliano
Prof Tibaijuka – Nyumba
Cristopher chizza – kilimo
Magembe – Maji
Mwakyembe – uchukuzi
Dr fenela mkangara – Habari vijana na michezo
Kaigasheki – Maliasili na utalii
Kidogo – Viwanga na Biashara
Fedha – William
Sospter – Madini
Mwandyosa – Asiye na wizara maalumu – Ikulu




Wasira -anaendelea
Kombani -Utumishi
Mkuchika -Utawala bora
Samia -anaendele na Muungano
Tereza- anaendelea na Maziria
Nagu -anaendelea
Lukuvi -anaendelea
Ghasia -Tamisemi
Sitta anaendelea
Nahodha -Ulinzi
Magufuli- anaendelea
Mwinyi -Afya
Kawambwa enaendelea
Simba -anaendelea
Membe- anaendelea
Chikawe- Katiba na Sheria
Nchimbi -Mambo ya Ndani
Mathayo anaendelea
Kabaka anaendelea
Mbarawa anaendelea
Tubaijuka anaendelea
Chiza -Kilimo
Mahembe- Maji
Mwakyembe -Uchukuzi
Mkungara -Habari
Kagasheki -Maliasili
Kigoda- Viwanda
Mgimwa -Fedha
Muhongo -Nishati
Mwandosya hana wizara maalumu
Mnaibu:
Kitwanga  VP
PM office  Majaliwa na Mwanri
Kazi Makongoro- Naibu
Malima- Chakula
Home- Silima
Teu -Viwanda
Nagoro -anaendelea
Lwenge -Ujenzi
Mahadhi -Nje
Medeye -Ardhi
Ummy- Jamii
Mulugo -Elimu
Juma- EA
Nyalandu -Maliasili
Rashid- Afya
Simbachawene -Nishati
Mkuya -Fedha
Makambo- Sayansi
Tizeba -Uchukuzi
Makala- Habari
Mahenge- Maji
Masele- Nishati Madini
Kairuki -Sheria
Mbene -Fedha








MAGAZETI YA IJUMAA

Kipanya Leo

Reactions::

Magazeti Leo Ijumaa















Reactions::

KEKI YA CCM


Keki Yenye Rangi Za CCM Yakataliwa 

Halima Mdee Mbunge wa Kawe akigeukia pembeni na kuonyesha ishara ya kukataa kuigusa keki ya Shay Rose Banji huku akicheka.

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa Tiketi ya Chama cha Mapinduzi waliangua Vicheko pale wenzao wa CHADEMA walipoikwepa kuigusa nakuila Keki ya Birthday ya Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Shy Rose Banji wakati wa tafrija yake iliyofanyika Nyumbani Longe Jijini Dar es Salaam.
Wabunge hao wa CHADEMA  ni Halima Mdee (Kawe) ambaye anaonekana picha ya juu akiikataa keki hiyo iliyotolewa na Wakurugenzi wa Nyumbani Longe, Gadna G Habash na Mkewe Lady Jay Dee, huku Mbunge wa Viti Maalum, Lucy Kiwelu picha ya chini nae akijificha asiitazame kwa karibu.
 
Wabunge hao waliigwaya Keki hiyo kutokana na jinsi ilivyopambwa rangi za CCM.

Huku Wabunge wa CCM wakishangilia wakimtaka Halima Mdee aongoze Ukataji wa Keki hiyo ambayo ilitolewa baada ya keki ya awali iliyoandaliwa na Baby Girl Shy Rose kuliwa, ilishindikana kuliwa na kuhifadhiwa.
 
Watu mbalimbali walihudhuria tafrija hiyo ndogo wakiwepo Wabunge, wanasiasa, Wasanii muziki, Watangazaji na Wanahabari ambapo kila aliye simama kuongea alimpongeza sana Shy Rose kwa kuwa Mpambanaji wa Ukweli katika kutafuta kile anachotaka na kumuombea kwa Mungu amuongoze vyema katika kazi yake

RAIS KIKWETE AMTEUA JAMES MBATI KUWA MBUNGE

JK ampa ubunge James Mbatia


*Wamo Profesa Muhongo, Bi. Janet Mbene
*Watabiriwa kuwemo kwenyea baraza jipya
*Nchimbi awaomba Watanzania wamuombee
*Tibaijuka, Magufuli nyota zao zang'aa

WAKATI Rais Kikwete anatarajia kufanya mabadiliko katika baraza kake la mawaziri wakati wowote sasa, jana amemteua Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia, kuwa mbunge.

Mbali na Bw. Mbatia, Rais Kikwete amemteua Profesa safi Profesa Sospeter Muhongo, Bi. Janet Mbene, kuwa wabunge. Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari jana Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu, ilieleza kuwa Rais Kikwete amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa mamlaka ya uteuzi aliyopewa.

"Rais Kikwete amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa mamlaka ya uteuzi aliyo nayo chini ya Ibara ya 66(i) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Uteuzi huo umetafsiriwa na wachambuzi wa masuala ya kisiasa kuwa watu hao wanaandaliwa kuwa mawaziri, hasa ikizingatiwa kuwa Rais anatarajiwa kufanya mabadiliko ya baraza lake wakati wowote kuanzia sasa.

Profesa Muhongo ambaye ni mtaalam wa masuala ya madini Geology anatabiriwa kukabidhiwa kuongoza Wizara Nishati na Madini, huku nafasi za wengine walioteuliwa zikiwa bado kitendawili.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana Mhadhiri wa Kitivo cha Sayansi za Siasa katika Chuo Kikuu cha SAUT, Profesa Mwesiga Baregu, kuhusu uteuzi huo, alisema; "Anawaandaa kwa ajili ya kuwaweke katika baraza lake la mawaziri."

Profesa Baregu alisema alisema baraza la mawaziri la sasa limepwa ndiyo maana ameamua kuchukua watu kutoka nje ya CCM. Alimshauri Rais Kikwete, kuteua baraza la mawaziri lenye sura mpya na watu wachache na wenye uwezo wa kufanyakazi.

Alitaja sifa nyingine ambazo anataka mawaziri wapya kuwa nazo kuwa ni uaminifu, wawajibikaji, uadilifu na wenye kuleta tija kwa wananchi wanaowatumikia.

"Akichagua wale wale wa zamani hakutakuwa na mabadiliko yoyote," alisema Profesa Baregu. Alishauri mabadiliko hayo ya baraza yafanyike haraka  kwani kuwaacha wanaotuhumiwa kwa kushindwa kuwajibika kuendelea kuwepo ofisini kunaweza kuwapa mwanya wa kupoteza vielelezo pindi watakapofikishwa kwenye vyombo vya sheria.

"Mimi namshauri rais kufanya mabadiliko haraka iwezekanavyo, kwani kuendelea kuwepo ofisini kwa mawaziri hao ni tatizo na mambo yanaweza kuharibika kwa kuwa wana uwezo wa kuchukua vielelezo na kupoteza ushahidi," alisema.

Hata hivyo alisema  kufanya mabadiliko pekee hakutasaidia bali  kinachotakiwa ni kuwatendea haki mawaziri hao kwa kuwafikisha mahakamani ili watakaobainika.

Alisema mbali na kubadilisha baraza la mawaziri, pia anatakiwa kuwachukulia hatua wote waliohusika wakiwemo makatibu wakuu wa wizara kama wanahusika.

Alisema upotevu wa fedha ni matokeo ya kukosekana kwa uwajibikaji miongoni mwa mawaziri hao. Alipoulizwa ni mawaziri wapi wanafaa kubaki kwenye safu mpya itakayoundwa, alisema atatoa maoni yake baada ya uteuzi.

Naye, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Dkt. Helen Kijo- Bisimba, alisema kubadilisha mawaziri si suluhuhisho kukabiliana na tatizo la viongozi kutowajibika.

Alisema kuwa suluhu ni kuwawajibisha wale wote waliohusika na  kwa kuwfaikisha mahakamani ili haki itendeke.

Kuhusu makatibu wakuu wambao ndio watendaji, Dkt. Kijo-Bisimba alisema kuwa mawaziri hao walitakiwa kuwawajibisha makatibu wakuu pale wanapoona kwamba hawarishishwi na utendani wao wa kazi kwa kuwa wao ndio wapo nafasi za juu kiutendaji.

Mwenyekiti wa Chama cha PPT-Maendeleo, Bw. Peter Mziray, alisema wabunge wamemweka Rais Kikwete kwenye kona mbaya, hivyo ni lazima afanye mabadiliko kwa kuteua mawaziri ambao wananchi wanawaamini.

Pia alishauri baraza atakalounda Rais Kikwete, liwe dogo, kwani la sasa ni kubwa kiasi kwamba inawezaka wakati mwingine akashindwa kuwafahamu.

"Ndiyo maana waziri anaweza kuwa na mali nyingi, lakini akashindwa kufahamu kwa sababu hana muda wa kuwafuatilia," alisema Bw.Mziray.

Aliwataja mawaziri wanaofaa kuwemo kwenye baraza hilo kuwa ni Profesa Anna Tibaijuka, Dkt. John Magufuli, Dkt. David Matayo, Bw. Bernard Membe na Bw. Shamsa Vuai Nahodha.

Wakati huo huo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emanuel Nchimbi, amewaomba Watanzania kumuombea ili aweze kuteuliwa tena kurudi kwenye baraza la mawaziri.

Alisema bado ana moyo wa kuwatetea Watanzania katika mambo mbalimbali ili kuijenga nchi hii.

"Bado ninahitaji kuwasaidia Watanzania wenzangu na ninawapenda, ndiyo maana leo hii tena muda kama huu ambapo mawaziri wengi wapo katika sala za kumuomba Mungu wao ili waweze kupita tena, lakini mimi nimeamua kuja kwenu kwa ajili ya upendo wangu na ni moja ya kazi yangu,"alisema, Dkt. Nchimbi.

Aliongeza kusema kuwa angeweza kumtuma hata mwakilishi wake ili afike katika hafla ya uzinduzi wa mwongozi wa wamiliki na mameneja wa vyombo vya habari, lakini kwa kuwa anafahamu maana yake, ndiyo maana ameamua kufika mwenyewe.

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT) Bw. Regnald Mengi alimpongeza Dkt. Nchimbi kwa ujasiri wake wa kufika katika uzinduzi huo wakati mawaziri wengine hadi hivi sasa wapo matumbo joto wakiangaika huku na kule ili majina yao yaweze kupitishwa.

"Nakupongeza Dkt. Nchimbi kwa ushujaa ulioonesha ni mkubwa na mawaziri wengi sasa hivi matumbo joto kwa ajili ya kusikiliza kitakachotokea, tunakuona ni jasiri, "alisema Bw. Mengi.
 
SOURCE MAJIRA



WASANII WARIKODI MBONI YANGU

Wema aliwakilisha waigizaji wa filamu
Wimbo huo ni kwa ajili kumchangia Sajuki