Wednesday, April 18, 2012

KAJALA ASOMEWA MAELEZO YA AWALI



Na Rehema Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jana ilimsomea maelezo ya awali msanii wa Filamu nchini, Kajala Masanja na mumewe Faraja Mchambo baada ya upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo.

Washatakiwa hao walisomewa maelezo hayo jana na wakili wa serikali kutoka  Takukuru, Leornad Swai mbele ya Hakimu Sundi Fimbo anayesikiliza kesi hiyo.

Baada ya kusomewa maelezo hao washtakiwa hao walikiri mahakamani kuuza nyumba iliyokuwa chini ya uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leornad Swai aliwasomea maelezo hayo ambapo washtakiwa walikiri kuwa ni mume na mke halali wa ndoa  na kwamba walishirikiana kuuza nyumba hiyo kwa Emiliana Rugarulila.

Mchambo alikiri kwamba nyumba hiyo ilikuwa chini ya uchunguzi wa Takukuru na kwamba kabla hajafunguliwa mashtaka hayo alikuwa mtumishi wa Benki ya NBC.

Kadhalika, Mchambo amekiri kuhusika na akaunti za Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) lakini hakufanya utakatishaji wa fedha haramu kupitia akaunti hizo.

Katika hatua nyingine , Kajala na Mchamba walikana kupokea amri (notes) kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikiwataka kutojihusisha na chochote ikiwemo kuuza nyumba hiyo kwa sababu ilikuwa chini ya uchunguzi wa Takukuru.

Aidha, wamepinga kushirikiana kuuza nyumba hiyo iliyozuiliwa kuuzwa na kwamba hawakwenda kinyume na amri iliyotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Wakili Swai alidai kuwa baada ya washtakiwa kukana baadhi ya maelezo hayo, upande wa mashtaka unatarajia kuita mashahidi 13 na kuwasilishwa vielelezo tisa dhidi ya mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao.

Katika kesi hiyo, washtakiwa wanadai  kula njama  kinyume na kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 ambapo washtakiwa wote kwa pamoja  walitenda kosa hilo la kula njama la kuamisha umiliki wa nyumba  iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam.

Shtaka la pili ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo  kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007.

Ilidai shtaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda  siku hiyo ya Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijiua ni kinyume na sheria hiyo.

Kesi hiyo itaanza kusikilizwa ushahidi wa upande wa mashtaka Aprili 30, mwaka huu.

Soma Majira

Tuesday, April 17, 2012

OLE MILLYA ATUA CHADEMA

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha atua CHADEMA



MWENYEKITI wa UVCCM, Mkoa wa Arusha,kwa miaka mitano, James Ole Millya,ametangaza kujiuzulu nafasi zote kuanzia Taifa hadi Mkoa na kutangaza kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa madai kuwa CCM imefilisika kimawazo na haitoi matumaini kwa watanzania.

Aidha alisema hawezi kuendelea kupanda gari lenye pancha lukuki, hivyo ameamua kupanda gari lisilo na pancha na lenye kutoa matumaini mapya kwa watanzania.

Hayo ameyasema leo, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye Hoteli ya Kibo Palace, iliyopo Jijini hapa.

Amesema mara nyingi alikuwa akikemea mambo ambayo yanaweza kubomoa chama cha CCM kwa upendo, lakini alikuwa akipuuzwa kwa sababu ya chama hicho kuwa na kikundi cha wenyewe.

“Mimi nanukuu maneneo ya Nyerere kuwa alishawahi kusema CCM sio mama yangu na mimi pia CCM sio mama yangu na natangaza rasmi, kuondoka ndani ya chama hiki na najiunga na Chadema, sababu ndicho chama chenye kuleta tumaini jipya kwa watanzania,”alisema.

Ametaja nafasi alizoachia ngazi ni pamoja na Mjumbe kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa, Mjumbe kamati ya siasa Mkoa na Mjumbe Halmashauri Kuu CCM Mkoa.

Amesema kuwa inasikitisha kuona Vijana wa UVCCM Mkoa wa Pwani, wanatoa matamko kuwa Rais ajaye 2015 hatatoka kanda ya Kaskazini na anayemfahamu ni Rais peke yake ambaye ni Jakaya Kikwete.

Millya alisema cha kusikitisha pale alipokemea kauli hiyo alipuuzwa na hadi sasa Ikulu haijawahi kutoa kemeo kwa Vijana hao na wala kukataza kauli hizo kutolewa, jambo lililompa jibu kuwa Ikulu inahusika kwa namna moja au nyingine na kauli hiyo.

Aidha alisema kuna Vijana wengi walioko ndani ya CCM wakiishi kwa matumaini ya kusubiri kuteuliwa nafasi ya Mkuu wa Wilaya kama sio Mkoa, ila yeye hawezi kuishi kw amatumaini kama muathirika wa Ukimwi.

Hata hivyo alitoa wito kwa Vijana wote wenye nia ya dhati na mapenzi mema ya nchi yao, kumfuata Chadema ambako kunatoa tumaini jipya la maisha ya watu.

Sunday, April 15, 2012

lady- Jay dee AIIBUKA MWIMBAJI BORA WA KIKE KTMA 2012 KTMA


DIAMOND AIBUKA MSHINDI WA MTUNZI BORA ,MTAYARISHAJI BORA NA VIDEO BORA YA MWAKA 2012

AKIWA NAK HALID CHOKORAA KABLA YA KUANZA KUIMBA  KTMA 2012

BARNABA AWA MTUNZI BORA WA NYIMBO WA KIUME KTMA 2012


HAYATI REMI ATUNUKIWA TUZO YA KUENDELEZA MUZIKI TANZANIA


TUZO ZA KTMA 2012 MLIMANI CITY JANA USIKU

MPOKI NDANI YA NYUMBA
WASHERESHAJI MC, MILAJI NA VANESSA
KHADIJA KOPA MUME WAKE NA WATOTO WAKE
KHADIJA KOPA AKITUMBUIZA 


BIBI CHEKA KATIKA POZI KTMA 2012


  
WATOTO WA KHADIJA KOPA WAKISHUKA JUKWAANI BAADA YA KUTAMBULISHWA NA MAMA YAO



V


 ALI  KIBAA AKIPOKEA TUZO YA WIMBO BORA WA ZOUK RHUMBA KUTOKA KWA DINA MARIOS  WA CLOUD RAINFRED  MASAKO WA ITV



 MTUNZI WA DANCEHALL QUEN DARLIN  AKIFURAHIA TUNZO