Tuesday, February 28, 2012

KAMA UNAMPENDA YESU KRISTO HALAFU HUMTAMBU MAMA BIKIRA MARIA HUO NI UONGO

Biblia ikisomwa kiholela na bila kuelekezwa na wajuzi, basi wengi huipotosha. Mtume Petro anatuonya katika 2 Peter 16-18.


 Uyasome aliyoyaandika mtume huyu . Ni kwa sabab...u hiyo basi wengi wanashundwa kumng’amua Bikira Maria katika Biblia.


Kwa MKRISTO yeyote, akisema anampenda YESU lakini hampendi au hamtambui Mama Bikira Maria huyo ni MWONGO.

Katika amri ya nne ya Mungu “Muheshimu Baba na Mama yako ...” tunaalikwa kuwaheshimu wazazi sasa kama wewe ni rafiki yangu unanipenda mimi ila humuheshimu wala kumpenda mama yangu, urafiki wetu utakuwa ni wa UWONGO.Yesu ndie aliyeweka amri kumi na asingekuwa wa kwanza kutokumheshimu mama yake na kumfanya BAHASHA.

Na ndio maana ukisoma biblia utaona tangu mwanzo wa salamu ya malaika mama Maria alijulikana tayari kama Malkia kwakuwa yeye ni mama wa MFALME YESU.

Maria ni malkia:-Ukisoma pale bikira Maria anamtembelea Elisabeth, utaona kuwa Elizabeth alijazwa na roho mtakatifu akasema “why should I be honoured with a visit from the mother of my lord?”- nawezaje kutembelewa na mama wa bwana wangu?
Sasa katika dini ya kiyahudi, Judaism, mama wa mfalme aliitwa malkia na hukuweza kumuita mtu yeyote “lord”- bwana isipokuwa ni mfalme. Elisabeth alivyomuita Maria “mama wa bwana wangu” alimaanisha mama Bikira Maria kuwa ni malkia. Soma Lk 1:43

MAMA maria aliambiwa na Mungu kupitia malaika gabrieli kwamba “umebarikiwa kuliko wanawake wote” sasa Yesu alipokuwa akitoa mheri nane pale Mlimani “Heri wenye moyo safi....” Heri zote hizo Mama Bikira Maria anazo kwahiyo ahadi zote ambazo Yesu amezitaja hapo, mama yetu Bikira Maria anazo. Sasa utakapomchukulia Maria kana kwamba ni aliwekwa tu kama boti ya kuzaa Yesu alafu ikatelekezwa baharini basi tunamfanya Yesu MUONGO.

Watu wanahoji mbona Bikira Maria hajatajwa sana katika biblia? Heshima aliyopewa bikira Maria ni kubwa sana na ukitaka kujua umuhimu wake uangalie matukio makubwa ya ukombozi mf.

1.Utabiri wa Ukombozi: Mwanzo 3:15 Nitaweka uadui kati yako na mwanamke na kati ya kizazi chako na cha MWANAMKE

2. Alipotenda muujiza wa kwanza: Yohane;2:4 Kisha Yesu akasema “WOMAN, what do you want from me?- MWANAMKE nina nini nawe? Kwanini Yesu hakumuita mama? Je hakumuheshimu? Hapana alikuwa anamkumbusha Maria kwamba “Muda wangu wa kufanya miujiza bado, kwani nitakapoanza kufanya miujiza, hutakuwa tena mam yangu peke yangu bali mama wa wanadamu wote wanaosubiria ukombozi.

Alimkumbusha kwamba yeye ni mwanamke wa Mwanzo 3:15 ambae ana uadui na nyoka”. Mama Bikira Maria hali akitambua hayo alimruhusu mwanae kwenda public ilihali akijua kwamba nay eye mateso kwake yanaanza.

3.Katika kilele cha ukombozi (At the climax of God’s ministry) John 19:26 “Woman, this is your son”- MWANAMKE, tazama mwanao. Hapa katika kilele cha ukombozi, Yesu kupitia john anaitambulisha dunia kwamba huyu ndie mwanamke aliyetajwa toka mwanzo na toka katika harusi ya Kana.

 Ndugu zanguni, Yesu anampenda mama yake kuliko nini sijui. Ukitaka kumjua Yesu zaidi, muombe mama yake akufundishe, kwani yeye anamfahamu mwanae vizuri.

 Alimogesha, alimfulia nguo, alimbembeleza alipolia, alishuhudia mwanae akisulibiwa uchi wa mnyama, na pia aliipokea maiti ya mwanae ikiwa imepondwapondwa na haitamaniki

.Kama unadhani Mungu ni katili kuoana huyu mama alivyoteseka alafu amuache aozee kaburini, basi utakuwa haumfahamu MUNGU vizuri.

AHADI ZA YESU KWA WAFUASI WAKE
1.Kushiriki ushindi wake(kifo), 2. Kushiriki utukufu wake(ufufuko)
Mama Bikira Maria alikuwa ni mfuasi wa kwanza wa Yesu