Wednesday, February 22, 2012

SIKU YA MAJIVU

TUMSIFU YESU KRISTO

LEO NI SIKU YA MAJIVU MIMI NAKWENDA KUSALI KAWE
TUMWOMBE MUNGU ATUSAIDIE KUTUBU DHAMBI ZETU ILI TUWEZI KUFIKA MBINGUNI .

SIKU YA LEO INATUKUMBUSHA KWAMBA SIKU MOJA TUTAKUFA TUJIANDAYE MAPEMA

TUMSIFU YESU KRISTO


 Mtoto akipakwa majivu





Waumini zaidi ya bilioni moja wa madhehebu ya katoliki na waothodox ulimwenguni kote pamoja na wakristo kwa ujumla leo wameanza mfungo wa kwaresma.


siku arobaini za kujinyima na kujitesa kwa ajili ya maandalizi ya ufufuko wa Bwana Yesu.


Hili ni jambo la imani na limedumu kwa zaidi ya milenia mbili sasa.Wakristo huombwa na Kanisa kufunga kabisa siku ya jumatano ya majivu ambayo ilikuwa leo.

Kuna theolojia kubwa na ngumu juu ya tendo hili la imani.


Kufunga chakula na kujinyima anasa na vitu tunavyovipenda ili kuungana na wenye shida wakati huu.Naam tunategemea kuona matendo mema wakati huu na kwamba yatakuwa mazoezi mema ya kiroho na yataendelea hata baada ya pasaka.


 Kuna kupakwa majivu katika paji la uso na maneno tubuni na kuiamini injili husemwa ambamo waumini hujibu amina wakikumbushwa juu ya umuhimu wa kumrudia Mungu na kwamba tumetoka katika mavumbi na tutarudi kuwa mavumbi.Rangi za Zambarau hutumika zikiwa na maana ya toba.

Naam nasi Mjengwablog tunawatakia Kwaresma njema.