Monday, April 23, 2012

LULU ATINGA MAHAKAMANI YA KISUTU TENA

Mshtakiwa Elizabeth Michael |(17), ' Lulu'  (mwenye nguo nyekundu, )akiteremka ngazi huku akiwa chini ya ulinzi mkali baada ya kupandishwa Kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo Aprili 23.2012 ambapo kesi hiyo  ilikuja kwa ajili ya kutajwa.  Kwa mujibu wa Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Rita Tarimo  ni kuwa upelelezi bado haujakamilika na mtuhumiwa kurudishwa rumande hadi Mei 07 mwaka huu itakapotajwa tena.